
Radio Kaya ni kituo cha redio kinachotangaza katika Kiswahili na lahaja za Kimijikenda (Kidigo, Kigiriama na Kiduruma) katika eneo la Pwani la Kenya. Kilianzishwa Julai 2007 na kinalenga kuelimisha, kuburudisha na kuwaarifu wasikilizaji kuhusu utamaduni wa pwani. Kinasikika katika masafa 93.1 FM Mombasa, 99.7 FM Malindi, 94.9 FM Kilifi na 94.9 FM Lunga Lunga.